Update; Msafara wa Rais Magufuli sasa unaelekea Mirerani, karibia Runinga yako ushuhudie matukio live kupitia TBC sasa! Mkuu wa Mkoa wa Manyara , Alexander Mnyeti anaingia kutoa salamu na kuwatambulisha viongozi mbalimbali wa Serikali na wa Kijeshi na wadau wengine waliohudhuria uzinduzi huo Mkuu wa mkoa anamshukuru Rais Magufuli kwa ujenzi wa ukuta huo ambao utazuia utoroshwaji wa madini na kuokoa mapato mengi Anasema pia wachimbaji wadogo awali walikuwa hawalipi kodi kabla ya ujenzi wa ukuta huo ila sasa wameshaanza kulipa Pia gari la kubebea wagonjwa katika mji mdogo wa Mrererani limenunuliwa na pia wizara ya maji imeanza kuchimba visima kwa ajili ya kutatua tatizo la upatikanaji wa maji. Mkuu wa jeshi la kujenga taifa (JKT) Martini Busungu anatoa taarifa ya ujenzi wa ukuta huo, anaanza kwa kutambua uwepo wa viongozi wa kiserikali na kijeshi waliohudhuria uzinduzi huo Anamshukuru Mkuu wa majeshi ya Ulinzi, Evance Mabeyo kwa kuanza kutoa maagizo juu ya ujenzi wa ukj
Comments
Post a Comment