Posts

Showing posts from March, 2018

TLS Wamvimbia Mwanasheria mkuu wa Serikali, yasema uchaguzibutafanyika kwa kanuni za zamani

Image
Chama cha Wanasheria cha Tanganyika Law Society (TLS) kimesema uchaguzi wa viongozi wa TLS utafanyika kwa muongozo wa kanuni za zamani na si mpya ambazo zimetolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.Kauli hii imetolewa katika kipindi ambacho wanachama kadhaa wa chama hicho wamejitokeza kutangaza nia ya kuwania nafasi ya Uraisi wa TLS, Fatma Karume na Godwin Ngwilimi ni moja kati ya wanachama wa TLS ambao wameonesha nia ya kurithi kiti hicho cha uraisi ambacho sasa kipo chini ya Tundu Antipas Lissu. Bwana Ngwilimi amesema wao kama viongozi wa TLS wako tayari kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya kanuni hizo kama serikali itashinikiza kanuni mpya zitumike ndani ya TLS.Nae Fatma Karume yeye amejikita zaid kwenye utetezi wa haki za binadamu hasa Police brutality, ameelezea mfano wa Polisi kumshikilia mtuhumiwa kituoni kwa siku 14 bila kumpeleka mahakamani, anasema TLS ndo chombo pekee cha kuhakikisha nchini kunakuwa na "Rule of Law" hivyo akiwa Rais atapambana na mambo hayo. ...

Saed Kubenea apeleka hoja binafsi bungeni kushinikisha kupatikana Tume Huru ya Uchaguzi.

Image
Dar es Salaam. Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amesema amepeleka bungeni barua ya kusudio la kuwasilisha hoja binafsi ya kuwa na chombo huru cha kusimamia uchaguzi. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Machi 11,2018 Kubenea amesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) si chombo huru cha kusimamia uchaguzi. Amesema barua hiyo aliiwasilisha Alhamisi Machi 8,2018 katika ofisi ya Katibu wa Bunge mjini Dodoma. Kubenea amesema uchaguzi kusimamiwa na Tume isiyo huru inaweza kusababisha machafuko. "Hatuwezi kuacha hali hii iendelee, vurugu zimekuwa zikitokea kwa sababu ya kuwa na Tume ya aina hii, tunataka chombo huru," amesema. Amesema tangu nchi iingie katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 uchaguzi umekuwa ukifanyika kwa kusimamiwa na Tume isiyo huru.

Msafara wa Humphrey Polepole wapatwa na ajari mbaya mkoani Kigoma

Image
Msafara wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Hamphrey Polepole umepata ajali katika eneo la kijiji cha Nyamidaho, Kata ya Makere wilayani Kasulu mkoani Kigoma leo. Ajali hiyo imehusisha gari aina ya Toyota V8 yenye namba T150 CWE iliyokuwa ikiendehswa dereva aliyefahamika kwa jina moja la Kibuta wakati wakielekea katika ziara ya kiongozi huyo wilayani Kakonko, Kigoma.

Dkt Azaveri Lwaitama na Katiba Mpya

Image
Inabidi tutofautishe kati ya dhana tatu; i) Dhana ya Maendeleo: Wananchi wanahitaji maendeleo, lakini maendeleo ni maendeleo ndani ya Uhuru. Sio Maendeleo wakiwa wanaswagwa kama mateka, vingnenvyo wangewatafuta Wajapani Wajerumani waje hapa wawapige bakora ili wawe na majengo. Wananchi wanataka maendeleo ya watu, maendeleo ya kupata uhuru zaidi. ii) Dhana Dola: Je ni dola ya kuchukulia watu mateka au ni dola la wachi huru amabo wamelidhia mamlaka fulani kwa watu ambao wanafanya kwa niaba yao?. iii) Dhana ya Chama: Chama ni kitu kinachoshawishi, ni chombo cha kushawishi watu sio cha kuwatisha. Sio chama kinachosema usipochagua huyu maendeleo hayatakuja kwako, usipochagua huyu utashughulikiwa. Kikifanya hivyo sio chama tena bali chama dora. Ni kikundi cha watu kimekamata dola halafu kinatumia chama. Sio chama kuwashawishi watu bali kuwatisha kwa sababu watu wanataka kubaki hapo hapo walipo. Hoja hapa ni kwamba ukishafika mahali ambapo chama kilichokuwa cha ukombozi, kime...

Ni makosa kupitisha siku nne bila ya kumuingilia mkeo

Image

Maamuzi ya MCL baada ya kutopatikana Mwandishi Azory

Image